TAMTHILIA: CPL (CERTIFIED PERSON OF MY LIFE) sehemu ya 01
TAMTHILIA: CERTIFIED PERSON OF MY LIFE (CPL)
(MTU ALIETHIBITISHWA KWA MAISHA YANGU)
MWANDISHI: MANSHINE
Email address: manshinef@gmail.com
instagram: @manshynee facebook @let us shine
Episode 01.
VENUE:
Ilikua
ni muda wa kipindi cha ujasiriamali kwa wanafunzi wanaosomea biashara.,
lecturer (mwalimu wa chuo) akiwa mbele ya venue akifundisha. Kutokana na ukali
wa lecturer yule darasa lilikua kimya sana hali iliyopelekea wanachuo kuwa
waoga kwasababu walishaambiwa katika kipindi chake kuleta fujo au kelele ni
sawa na kujiondoa chuoni hapo.
Frank
akiwa ni mmoja wa wanachuo alikua makini sana kusikiliza. Ilifikia hatua akawa
anatikisa kichwa kuonyesha jinsi gani alikua akielewa katika kipindi hicho.
Wakati kipindi kikikaribia kuisha, mkufunzi (lecturer) aliuliza swali…
“wanafunzi
Nani anapenda kuwa mfanyabiashara., na kwanini? Na mtaji utaupata wapi?
loveness
akanyosha mkono, akaambiwa ajibu swali…
LOVENESS:
mimi sipendi kuwa mfanyabiashara kwasababu biashara zina hasara nyingi, ni
ngumu kupata mtaji kwa sababu watu wengi wanaitaji fedha na fedha ni ngumu
kupatikana. Kabla mwalimu hajaongea chochote akaona mkono wa frank….
MWALIMU:
eeh frank nawe una jibu jipya? Ebu tupe jibu lako
FRANK:
mwalimu nataka nimjibu loveness, loveness unaposema hupendi kuwa mfanyabiashara
una maana gani? Na kama hupendi tuambie kwanini unasomea biashara?
LOVENESS:
mfanyabiashara ni sawa na mtu aliejiajili, sasa mimi nikijiajiri kuna faida
gani za kusoma sasa? Si nitakua tu nimepoteza fedha zangu. Sasa si bora
ningekaa nyumbani na hizo fedha za ada ningezitumia kama mtaji. Nasomea
biashara kwa sababu serikali itanipa ajira zinazohusu usimamizi wa biashara za
wananchi.
FRANK:
HAPANA, kumbe una mawazo finyu hivo. Tena wewe mwanachuo wa elimu ya juu
unaweza ukatupatia majibu kama hayo? Hata hiyo serikali haiwezi ikakuamini
kwasababu huwez ukaongoza wafanyabiashara wakati hupendi biashara.
LOVENESS:
kwani tatizo lipo wap? Jaman kila mtu ana ndoto zake. Humu ndani kuna watu
wanawaza kujiajiri na kuna wengine akina sisi hatuna mpango huo. Mimi nachoamin
baada ya ku graduate ni kusubili ajira tu. Na naamini nitaajiliwa. Siwez
kupoteza muda wangu na fedha zangu bure hata wale wenzangu walioko uko mtaani
si watanicheka?
FRANK:
loveness kwanza serikali ni nini? Unataka kusema serikali haifanyi biashara?
Hivi hujawai kusikia serikali inanunua au kuuza vitu kutoka nje? Tena ni juzi
tu tumemaliza topic ya international trade, unataka kusema ile topic hukuilewa
au?
LOVENESS:
kwan wewe unataka nini? Kama unaona jibu langu sio sahihi basi tupe lako kwa
sababu naona unapinga mawazo yangu. (aliongea loveness akiwa na uso wa hasira
na akaamua kukaa chini)
FRANK:
haina haja ya kupanic kwa sababu swali liko wazi kwa sisi wote ambao tunachukua
biashara. Mimi sijamaanisha kwamba sitaki kuajiriwa au sijamkataza mtu
kuajiriwa ila Kutokana na swali majibu ya dada etu love sidhani kama ni sahihi.
Mwanachuo alie kamili kifikra hawez kutujibu vile…... (kabla frank hajamaliza
kuongea loveness akasimama kwa hasira na kuongea)
LOVENESS:
kwahyo mimi sina fikra, sifai kuwa mwanachuo, unaamua kuni…. (kabla hajamaliza
kuongea akaanza kulia kwa kwikwi na akatoka nje kwa hasira bila hata kuangalia
nyuma).
Kulikua
na ukimya wa muda, kipindi hayo yote yanaendelea darasa lilikua kumya
kusikiliza, kuna nyuso zilionyesha huruma kwa loveness na kuna nyuso ziliona ni
kitu cha kawaida kimetokea…kwa upande wa frank alikua bado amesimama, alipotaka
kukaa mwalimu akamwambia inabid alijibu swali kwa faida ya waliobaki…...
FRANK:
Mimi napenda kuwa mfanyabiashara, hata kama ikitokea nikapata ajira selikalini
lakin sitoacha kufanikisha ndoto zangu za kuwa mfanyabiashara na ndio maana
niliamua kusomea kozi hii. Napenda biashara kwa sababu biashara iko popote iwe
ni sekta za umma hata zile binafsi, ailimia 99% za vipato vya watu ni biashara.
Kwa upande wangu biashara inatengenezwa na bidhaa pamoja na huduma za kijamii.
Hivo basi hata serikali inatengenezwa na biashara. Na kuhusu mtaji ni rahisi tu, kuna mikopo
kutoka bank na mshirika yatoayo mikopo, kuna akiba, kuna misaada kutoka kwa
watu wa karibu n.k
MWALIMU:
safi sana, nadhani hakuna asiyekuelewa. Na hii inaonyesha ni jinsi gani una
upeo wa kielimu hasa katika kozi yako ya biashara. Class see you next lecture.
Aliaga mwalimu na akaondoka darasani….
Baada ya
mwalimu kuondoka, huku nyuma yalibaki majadiliano kuhusu yaliyotokea, kuna
waliosema frank amekosea sana kwa kumdhalilisha loveness, kuna waliosema frank
ameongea sahihi. Ilikua ni kelele tu Kila mtu akiongea lake.
Baada ya
muda watu wakaanza kutawanyika hadi frank akajikuta yuko pekeake mule ndani.
Kwakuwa ilikua ni saa 6 mchana frank akaona ni bora ajisomee tu mule darasani
hadi mida ya saa saba ndo akale chakula. Akatoa ki note book chake akaanza
kukipitia, hakuwaza sana kuhusu yaliyotokea kwasababu aliona ameongea vitu
ambavyo mtu yeyote angeweza kuongea. Akiwa yupo busy na kusoma mara akaingia
Maria ambaye ni groupmate mwenzie.
MARIA:
frank vipi mbona pekeako humu class?
FRANK:
hamna nimeamua tu, nimeona nikiwa nasubir mda wa msosi, niwe napitia pitia
kidogo.
MARIA:
hivi una taarifa mwenzio kapelekwa hospital ya chuo?
FRANK:
mwenzangu gani?
MARIA:
si loveness baada ya kutoka class unaambiwa kaenda hostel na kilio, sie
tumetoka pindi tunafika hostel tunamkuta mtu kazidiwa ilibidi tumuwaishe
hospitali.
FRANK:
(KWA MSHANGAO) eeh lakin si alikua poa tu. Amezidiwa kivipi?
MARIA:
hospiali wanasema ni maumivu ya kichwa yalimzidi. Na inasemekana chanzo ni
wewe?
USIKOSE SEHEMU YA PILI....
Nimeipenda
JibuFutaHanifa
FutaNi nzuri jaman
JibuFuta